Mgonjwa auawa ndani ya wodi KNH - Citizen TV Kenya
Mgonjwa mwingine amefariki ndani ya wodi 7B katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta. Ripoti za awali zinaashiria kuwa mgonjwa huyo wa umri wa miaka 54 aliuawa akiwa kitandani alikokuwa amelazwa. Eneo hilo sasa limefungwa, maafisa wa DCI wakianza uchunguzi huku harakati za kumtambua mtu huyo zikiendelea.